MATUNDA YA MIDOMO NA MATOKEO YAKE


 Ibrahimu aliitwa baba wa mataifa mengi wakati huo hakuwa na mtoto,  Mungu huyasema yasiyokuwako kana kwamba yapo (Warumi 4:17)

Ni muhimu sana ujifunze kutamka au kukiri tofauti na hali inavyokulazimisha kukiri au kutamka, Mungu anasema "aliye dhaifu aseme mimi ni hodari" Yoeli 3:10

Watu wengi hawaamini kama nguvu ya kukiri au kutamka inatenda kazi kabisa, na Mungu anafuatilia mambo ambayo watu hutamka au kukiri

(Hesabu 14:26-28)

Aliwaambia wana wa Isareli kuwa "kama walivyonena masikioni mwake ndivyo itakavyokuwa yaani waliyoyatamka yatawapata"

Mungu huyaumba matunda ya midomo (Isaya 57:19)

Hivyo basi jizoeze kukiri au kutamka mambo mazuri hata kama hali halisi haifanani na unavyokiri.

Chapisha Maoni

0 Maoni