Wakati mwingine muombe Mungu akuinulie watu wa kukupenda.
Mungu alimpa Daudi mtu wa kumpenda aliyeitwa Jonathani mtoto wa Mfalme Sauli (1 Samweli 18:1-4)
Kutokana na upendo aliokuwa nao Jonathani kwa Daudi, Jonathani alivujisha taarifa za mipango iliyopangwa na Mfalme, mipango ya kumuangamiza Daudi (1 Samweli 19:1-7), Daudi alinufaika sana na upendo huo.
Jonathani alipokufa, Daudi wakati huo alikuwa Mfalme aliomboleza sana, soma maelezo ya maneno ya maombolezo ya Mfalme Daudi kuhusu Jonathani.
2 Samweli 1:26. Nimesikitika kwa ajili yako, Yonathani, ndugu yangu, Ulikuwa ukinipendeza sana; UPENDO WAKO KWANGU ULIKUWA WA AJABU, KUPITA UPENDO WA WANAWAKE.
✓Ni kweli hutapendwa na kila mtu ila UKIKOSA WATU WA KUKUPENDA UTAKOMA.
✓ Wakati mwingine muombe Mungu akuinulie watu wa kukupenda.

0 Maoni