KUHUSU NGUVU ZA KIROHO NYUMA YA BIASHARA


Nianze kwa kukujulisha kuwa hakuna biashara inayoendeshwa na mtaji peke yake, USIDANGANYIKE.

Kila biashara unayoiona hapa chini ya jua haijalishi ni kubwa au ndogo, kuna nguvu fulani za kiroho nyuma ya biashara hiyo, kuna nguvu fulani za kiroho zinazomsaidia mfanyabiashara au mjasiriamali huyo (Ufunuo wa Yohana 18:3,23)(2 Wafalme 4:1-7).

Nguvu hizo zinaweza kuwa nguvu za Mungu au nguvu za shetani, kwa hiyo kama unataka kuanza kufanya biashara, USIANZE KWA SABABU UNA MTAJI, TAFUTA NGUVU KWANZA.

Madhara ya kutegemea nguvu za shetani ni kwamba UHAI WAKO, UHAI WA WATU WAKO WA KARIBU UKO HATARINI KWA SABABU SHETANI SIO MWEMA, akikupa nguvu zake utaweka rehani nafsi yako pia utawaponza wengine.

Wanaotegemea kufanya biashara kwa kutumia nguvu za shetani wao wenyewe wanafahamu wanaishi katika mazingira magumu hata kama wanapata fedha nyingi, wako kwenye hatari kubwa, wanafanya mambo yanayowatesa sana.

Nashauri jipatie nguvu za Mungu zikusaidie kwenye biashara yako, nguvu za Mungu ni pamoja na mawazo ya Mungu, neno la Mungu, maarifa ya Mungu, hekima ya Mungu nakadhalika.

Nguvu za Mungu zitalinda biashara yako, zitakupa mvuto wa kibiashara, zitakupa mawazo, zitakupa akili za kukusaidia katika biashara.

Chapisha Maoni

0 Maoni