NYUMA YA MAFANIKIO


NYUMA YA MAFANIKIO YANAYOONEKANA kuna maumivu yasiyoonekana na gharama ambazo zimelipwa. 

Huwezi kufanikiwa hapa duniani kwa jambo lolote ikiwa hauko tayari kuumia na kulipa gharama.

👉Mwanamke ili azae lazima apate uchungu kwanza, katikati ya uchungu na maumivu mtoto huzaliwa, hata wanaojifungua kwa upasuaji nao hupitia adha ili mtoto azaliwe.

👉Unamkumbuka Nelson Mandela yule wa Afrika kusini, kabla hajafanikiwa kuwa Rais wa nchi alipitia nyakati zenye maumivu makali, hatimaye akaja kuwa Rais wa Nchi.

👉Unamkumbuka Mwl. Julius Nyerere wa Tanzania, kabla hajawa Rais wa Tanzania alipitia nyakati zenye maumivu mpaka kufika alipofika kisiasa.

IKO HIVI: Njia ya kuelekea kwenye mafaniko imesongwa na miiba, dhoruba na nyakati za maumivu hivyo basi lazima uwe tayari kuumia na kulipa gharama.

👆Hiyo ni kanuni ya kupata mafanikio katika jambo lolote hapa duniani.

Chapisha Maoni

0 Maoni