MUNGU ANAYEWASAIDIA WATU WAKE KUPATA NAFASI ZA KAZI


 Biblia haituambii kwa undani kama ile nafasi ambayo Mfalme Farao alimuweka Yusufu ilikuwa wazi au ilikuwa na mtu au ilikuwa nafasi mpya (Mwanzo 41:35-45).

Ila Biblia inatuambia Mfalme Farao alimuweka Yusufu kwenye nafasi ile kwa kuwa aliona jambo la tofauti ndani ya Yusufu (Mwanzo 41:38), Mfalme Farao hakutaka kujua kiwango cha elimu ya Yusufu, ujuzi alionao nakadhalika ila alimpa nafasi ile kwa sababu Yusufu ana Mungu.

IKO HIVI: Haijalishi nafasi za kazi zina watu au zimejaa, yamkini kazi hazipo, yamkini ajira hazitangazwi, YUPO MUNGU MBINGUNI AWEZAYE KUWATENGENEZEA MAZINGIRA RAFIKI WATU WAKE ILI WAPATE KAZI. 

●Ni Mungu aliyemtengenezea Daudi mazingira rafiki ya kupata kazi kwa Mfalme Sauli.

●Ni Mungu aliyemtengenezea Yusufu mazingira rafiki ya kupata kazi kwenye utawala wa Mfalme Farao wa Misri.

Chapisha Maoni

0 Maoni