FAHAMU HILI KUHUSU NDOTO


 Ndoto zingine unazoota ni mawazo anayokuwazia mtu au watu fulani na maamuzi watakayoamua kutokana na mawazo wanayokuwazia (yale yaliyomo kwenye moyo wa mtu au watu fulani).

Mungu hukufunulia au hukujulisha yaliyomo ndani ya moyo wa mtu fulani au watu fulani KUPITIA NDOTO.

Mungu hukufunulia na kukujulisha mawazo na maamuzi yanayotokana mawazo anayokuwazia mtu fulani au wanayokuwazia watu fulani KUPITIA NDOTO.

(Mwanzo 40:1-22)

Ndoto walizoota hao watumishi wa Mfalme Farao yalikuwa mawazo ya Mfalme Farao kuhusu hao watumishi na maamuzi atakayoamua kutokana na mawazo aliyokuwa anawawazia.

(Waamuzi 7:13-15)

Ukisoma andiko hilo utagundua kuwa ndoto aliyoota huyu mtu ilikuwa ni yale yaliyomo ndani ya moyo wa Gideoni (mpango wa Gideoni kushambulia maadui zao).

BAADHI YA NDOTO AMBAZO WATU HUOTA KUHUSU YALIYOMO NDANI YA MIOYO YA WATU

1. Kuota mtu fulani anakukimbiza.

2. Kuota mtu fulani anakupiga au unapigana na mtu fulani.

3. Kuota mtu fulani amekugeuzia kisogo.

4. Kuota unamuita mtu lakini hakujali kabisa.

Hizo ni baadhi ya ndoto ambazo hufunua yaliyomo ndani ya moyo wa mtu fulani au mioyo ya watu fulani.

NB: 

1. Si kila ndoto ni ya kupuuza, uwe makini.

2. Kama umeota ndoto usiyoielewa tafuta watumishi wa Mungu wakusaidie kwa kuwa KUFASIRI NI KAZI YA MUNGU.

3. Kupata tafsiri ya ndoto ni jambo muhimu sana katika kukusaidia kufanya maamuzi mbalimbali.

Chapisha Maoni

0 Maoni