Kuombea maeneo si jambo ambalo linakumbukwa
na watu wengi na matokeo yake maeneo yamekuwa na hali mbaya sana za kiroho,
unaposoma Biblia utaona Mungu aliwaambia wana wa Israeli “wautakie AMANI MJI
waliotoka” yaani wauombee amani mji wao maana mji unapokuwa na amani ndipo na
wao watapata amani kutokana na amani ya mji (Yeremia 29:7).
Mara nyingi tumekuwa tukisikia kuhusu
“utabiri wa HALI ya hewa” na katika utabiri wa hali ya hewa ndipo wataalamu
huwa wanatuambia kuwa eneo Fulani kutakuwa na hali Fulani kwa mfano joto kiasi,
mvua kiasi, mvua zinazoweza kuleta madhara n.k na wakati mwingine wataalamu
hutoa maelekezo juu ya namna ya kujikinga na hali ambayo inaweza kutokea
kutokana na hali iliyotabiriwa.
Ndivyo ilivyo hata katika masuala ya kiroho,
roho Fulani inapokaa juu ya eneo ghafla hali ya hali ya eneo inabadilika kabisa
itategemeana na roho iliyokaa juu ya eneo ni roho ya aina gani, na kama roho
hiyo haitokani na Mungu basi lazima hali itakayokuwepo juu ya eneo itakuwa hali
yenye madhara makubwa juu ya eneo na juu ya maisha ya watu endapo
haitashughulikiwa kwa njia ya maombi.
Ninaposema kuombea hali za kiroho za maeneo
ninalenga kushughulikia roho zinazopata nafasi ya kukaa juu ya eneo Fulani na
zinasababisha madhara katika mazingira na maisha ya watu kwa ujumla, tumekuwa
tukishuhudia mitaa, vijiji, kata, tarafa, wilaya, mkoa au taifa likiwa na sifa
Fulani kwa mfano unaweza ukasikia mtaa au kijiji Fulani kuna wachawi wengi au
kuna makahaba wengi au mabinti wengi huwa hawamalizi masomo au kuna wavuta
bangi wengi n.k chanzo kimojawapo cha matukio hayo ni hali za kiroho za maeneo
husika.
(Mwanza 1:1-2)
Ukisoma andiko hilo utakutana na sentensi hii
“Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa
maji” Biblia inasema Giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji maana yake ni kwamba ili giza
liondoke juu ya uso wa vilindi vya maji ilitakiwa kwanza Roho ya Mungu ije juu
itulie juu ya uso wa maji na baada ya Roho ya Mungu kuja juu ya uso wa maji
ndipo Mungu akasema “iwe nuru na nuru ikawa”. Ninachotaka uone hapo ni suala la
Roho ya Mungu na mazingira, kwa hiyo ni vema ujue hata roho za kishetani
zinaweza kukaa juu ya eneo na ghafla matokeo ya uwepo wa ile roho yataanza
kutokea kwenye mazingira na maisha ya watu kwa ujumla kutokana na hali ya
kiroho itakayotengenezwa na ile roho.
Badhi ya mambo
yanayotokea pale roho Fulani inapokaa juu ya eneo
à Hali ya
kiroho ya eneo huwa inatengeneza AINA FULANI YA WATU
Kwa mfano watu wachoyo, wasio wakarimu,
wafiraji, makahaba, wapenda rushwa n.k. Ukiona mtu anaitwa MASKINI ni vema ujue
kinachofanya aitwe hivyo ni HALI aliyonayo yaani UMASKINI ndio unatengeneza
watu MASKINI, kumbuka UMASKINI ni roho inayotokana na shetani, kwa hiyo kama
roho ya umaskini itakaa juu ya eneo tarajia kuona eneo hilo likikaliwa na watu
maskini.
(Matendo ya mitume 21:39)
Mtume Paulo anasema alitoka katika “MJI
USIOKUWA MNYONGE” unaweza ukajiuliza Paulo alikuwa anamaanisha nini kusema
kauli hiyo, ukisoma hilo andiko kwa haraka unaweza usione maana ya hiyo
sentensi lakini Mtume Paulo alikuwa anazungumzia hali ya kiroho ya MJI
aliotoka.
Kwa hiyo Paulo anataka wau wajue kuwa hali ya
kiroho ya eneo inatengeneza na aina Fulani ya watu na ndio maana Mtume Paulo
alikuwa mtu jasiri hakuwa mtu goi goi na ndio maana hata alipokuwa muuaji
alifanya kazi yake kwa uhodari mkubwa na hata alipokuwa mtumishi wa Mungu
alikuwa mtumishi mwenye uhodari na hata kuna mahali aliwaandikia watu “hatimaye
MZIDI KWA HODARI katika Bwana”. Kilichomtengeneza Paulo kuwa mtu jasiri ni hali
ya kiroho ya mji aliotoka.
Hali ya
kiroho ya eneo huwa inatengeneza AINA FULANI YA MATUKIO katika eneo husika.
Kwa mfano kuna maeneo mengine si ajabu kuona
ajali zikitokea mara kwa mara, wizi wa mara kwa mara, watoto kutupwa majalalani
n.k hayo yote yanasababishwa na hali ya kiroho ya eneo husika.
(Isaya 1:21-27)
Tunaona katika andiko hilo Mungu anasema kuwa
“MJI HUO ULIKUWA MWAMINIFU” lakini ghafla “MJI UMEKUWA KAHABA” ukisoma andiko
hilo kwa haraka unaweza usione maana ya andiko hilo lakini unaposoma andiko
hilo kwa msaada wa Roho Mtakatifu utagundua kuwa hapo awali uaminifu ulitawala
katika mji na kutokana na uaminifu wa mji ukapelekea na watu waliokuwa wanaishi
katika mji wakawa waaminifu, lakini baada ya muda “roho ya ukahaba” ikapata
nafasi juu ya mji, sasa angalia matukio yaliyoanza kutokea baada ya hali ya
kiroho kubadilika, nataka nikuonyeshe matukio machache;
(a)Fedha yao haikuwa na thamani(thamani ya
fedha ilishuka) hali ya kiroho ya mji ilipobadilika ghafla na thamani ya fedha
ikashuka, hili suala la thamani ya fedha kushuka si suala geni kwa kuwa
linaonekana hata leo unakuta sehemu nyingine mtu anakwenda na hela nyingi
sokoni lakini anarudi amenunua vitu vichache kwa kuwa thamani ya fedha imeshuka
na hicho ndicho kilichotokea hali ya kiroho ilipobadilika katika eneo lile (Isaya
1:22)
(b)Suala la kutenda haki likatoweka katika
mji, maana yake ni kwamba dhuluma ikatawala katika mji (Isaya 1:21)
(c)Viongozi wakaanza kuwa waasi na marafiki
wa wezi, viongozi wakaanza kuwa na marafiki mafisadi (Isaya 1:23)
(d)Rushwa ikaanza kutawala (Isaya 1:23)
Hayo yalikuwa baadhi ya matukio yaliyotokea
baada ya hali ya kiroho ya mji kuwa imebadilika.
Hali ya
kiroho ya eneo inaweza kuwafanya watu waliopo kwenye eneo hilo wakawa wanaota
aina Fulani ya ndoto kulingana na roho iliyokaa kwenye eneo
(Mwanzo 28:10-17)
Tunaona katika andiko hilo Yakobo alifika
mahali Fulani akalala na baada ya kulala akaota ndoto ambayo ilidhihirisha kuwa
Mungu yuko mahali pale, na baada ya ndoto hiyo Yakobo anasema hakujua kuwa
Mungu yuko mahali pale na Yakobo akahisi kwamba lile eneo ni LANGO LA MBINGUNI
kwa kuwa Mungu alijifunua kwake kwa njia ya ndoto.
Ninachotaka uone hapo ni kwamba roho Fulani
ikikaa juu ya eneo ghafla watu wa eneo husika wanaweza kujikuta wakiota ndoto
zinazofanana.
Hali ya
kiroho ya eneo huwa inatengeneza AINA FULANI YA TABIA
(Danieli 3:1-7)
Tunanona katika wilaya ya Babeli kuabudu
miungu ilikuwa ni jambo la kawaida kwa kuwa ilifikia hatua kuabudu miungu ikawa
tabia yao, hiyo yote ilitokana na hali ya kiroho ya eneo husika, tunaona akina
Shadraka na wenzake walipokuja kuonyesha tabia tofauti na tabia ya eneo husika
ghafla wakatangaziwa kuuawa.
(Mwanzo 20:1-3)
Tunaona watu wa lile eneo walikuwa na tabia
ya kuchukua wake za watu kwa nguvu na kulala ndio maana Ibrahimu akaona aseme
kuwa Sara ni dada yake na si mke wake kwa kuwa Ibrahimu aliogopa kuuawa kwa
kuwa watu wa lile eneo walikuwa na tabia ya kuua kila mwanamume mwenye mke
mzuri.
Kwa hiyo ni vema kila mwana wa ufalme ajue
anao wajibu wa kuomba kwa ajili ya mambo mbalimbali katika nchi na taifa kwa
ujumla.
0 Maoni