Mwaka 2016 tumeshuhudia Raisi wa Marekani
Donald Trump akibadilisha kabisa hali baada ya kutangaza hataki wageni katika
taifa la Marekani, ninachozungumzia mimi sisemi wageni wasiingie katika taifa
Bali ninachosema ni kwamba ni muhimu kuombea ujio wa wageni waingiao kwenye
taifa pamoja na safari za viongozi wa nchi na watu mbalimbali walio katika
nafasi za utawala.
Ni muhimu ukafahamu kuwa kuna safari za viongozi
wa nchi ambazo huwa zina ratibiwa na shetani ili kuliharibu taifa na njia hii
shetani anaitumia sana, kuratibu safari mbalimbali na ujio wa watu mbalimbali
katika taiga kumbuka habari za Yusufu kukimbilia Misri akiwa na Mariamu mkewe
pamoja na Yesu ilikuwa safari iliyoratibiwa na Mungu mwenyewe ili kumnusuru
Yesu asiangamizwe na Herode,kama Mungu kuna safari anaziratibu nimuhimu uelewe
kuwa hata shetani naye huwa anaratibu safari mbalimbali.
Kila safari huwa ina mambo mawili;sababu ya
kusafiri na matokeo ya safari kwa hiyo shetani anaporatibu safari anakuwa na
makusudi au sababu na pia anakuwa ameshapiga mahesabu juu ya matokeo ya safari
hiyo katika taifa.
(2 MAMBO YA NYAKATI 18:1-34)
Tunaona Mfalme Yehoshafati aliondoka au
alisafiri kwenda kumtembelea Mfalme Ahabu hiyo ilikuwa ni safari ambayo
iliratibiwa na shetani kabisa na utaona alipofika kwa Ahabu ghafla Mfalme Ahabu
anamshawishi Mfalme Yehoshafati ili amsaidie ili waende kupigana na maadui wa
Mfalme Ahabu.
Baada ya Mfalme Yehoshafati kukubali
kumsaidia Mfalme Ahabu kwenye vita yake jambo hilo halikumfurahisha Bwana
ghafla Mfalme Yehoshafati anapata msukumo wa kutafuta nabii ili wamuulize Bwana
kama waende vitani au wasiende.
MATOKEO YA SAFARI YA MFALME YEHOSHAFATI KWA
TAIFA LAKE
1.Wanajeshi walikufa(2 mambo ya nyakati 18:3)
Mfalme Yehshafati alipokubali kuwa atakwenda vitani kumsaidia Mfalme Ahabu
tunaona Ahabu anakwenda na jeshi lake na wanajeshi walikufa vitani na hata yeye
mwenyewe alinusurika kufa Bwana akamuokoa (2 mambo ya nyakati 18:31) chanzo cha
hayo yote ni safari, ni muhimu sana kwa maaskari kuwa waombaji kwa sababu wao
wanaishi kwa amri tu kwa hiyo lolote watakaloagizwa kufanya haijalishi ni jema
au baya lazima walifanye tu na hata unapoangalia maaskari wengi wa nchi mbalimbali
wanakufa Vitani kwa sababu ya mikataba iliyofanywa na viongozi wa nchi juu ya
masuala ya ulinzi na usalama na ukiangalia mikataba mingi kama si yote chanzo
chake ni safari.
2.Kuna familia katika taifa la Yuda
lililokuwa likiongozwa na Yeshoshafati zilibaki na mzazi mmoja yaani mama
tu(single parent family) hususani familia ambazo akina baba walikuwa
wanajeshi(2 mambo ya nyakati 18:3,28) Mfalme Yehoshafati alipeleka wanajeshi
vitani na wengine walikufa na hatimaye kwenye taifa zikabaki familia ambazo
hazina baba bali ni mama ameachwa kuongoza familia kwa hiyo safari ya Mfalme
Yehoshafati ilisababisha idadi ya wajane ikaongezeka katika taifa.
3.Baadhi ya familia zilijikuta kwenye hali
ngumu za kiuchumi hususani familia za wanajeshi waliouawa vitani,yote hayo
yalisababishwa na safari ya Mfalme Ahabu.
MATOKEO YA VITA KWA TAIFA LA SAMARIA
1.Taifa la Samaria lilipoteza Mfalme kwa
sababu Ahabu alikufa vitani(2 mambo ya nyakati 18:15,34)
2.Kuna familia katika taifa la Samaria
zilibaki na mzazi mmoja tu hususani familia za wanajeshi ambazo akina baba
walikufa vitani maana yake ni kwamba idadi ya wajane iliongezeka Samaria.
3.Wanajeshi wengi walikufa na uchumi uliyumba
si kwa familia tu ambazo zilipoteza wapendwa wao bali hata kwa taifa kwa sababu
vita inatafuna hata uchumi wa taifa.
(1 WAFALME 16:29-33)
Mfalme Ahabu alioa mwanamke ambaye alitoka
nje ya nchi na hii ilikuwa hatari kwa taifa la Israeli kwa sababu huyo mama
ndiye alikuwa mke wa Mfalme na wakati huohuo ni muabudu miungu na ndio maana ni
muhimu sana kumwombea mke au wake wa viongozi wa nchi kwa sababu ukiangalia
kuna mambo mengine yalifanywa na yezebeli na kwa hali ya kawaida ungeweza
kusema aliyefanya ni Mfalme kumbe si Mfalme bali ni mkewe.
MATOKEO YA SAFARI YA YEZEBELI KATIKA TAIFA LA
ISRAELI
1.Yezebeli mke wa Ahabu alimfanya Ahabu
ajenge madhabahu za miungu ya Baali katika taifa alilokuwa akiliongoza hivyo
basi Mfalme Ahabu akawa muabudu miungu(1 Wafalme 16:29-33)
2.Maisha yakaanza kuwa magumu kwa watumishi
wa Bwana, watumishi wa Bwana wakaanza kuuawa(1 Wafalme 17:13,19:2-10)
3.Taifa la Samaria likawa na wimbi kubwa la
manabii wa uongo(1 Wafalme 18:21-22) kumbuka manabii wa uongo wakiongezeka
katika taifa mafundisho ya uongo yanaongezeka na mafundisho ya uongo
yakiongezeka ghafla na imani za watu zinageuka kuelekea kwa miungu iliyotoa
mafundisho hayo kwa kuwa imani chanzo chake ni kusikia na imani za watu
zikielekea miungu,miungu ndio itaabudiwa katika taifa.
4.Yezebeli aliingia katika taifa la Samaria
na Miungu yake na ghafla hali ya mashaka ikatengenezwa ndani ya mioyo ya watu
na hivyo basi watu wakaanza kuishi kwa mashaka juu ya Mungu wa Israeli(1
Wafalme 18:21).
5.Yezebeli alipoingia Samaria ghafla mbinu
mpya za mauaji zikachukua nafasi katika taifa na wenye haki wakaanza kuuawa kwa
ajili ya haki zao na ukiangalia muhuri uliotumika kuua wenye haki ni muhuri wa
Mfalme lakini hakuweka mhuri Mfalme Bali aliyeweka muhuri ni mkewe na ndio
maana nikakwambia kuwa ni muhimu kuwaombea wake za viongozi (1 Wafalme
21:1-13).
MATOKEO YA SAFARI ZA WANAWAKE AMBAO WALIINGIA
KATIKA TAIFA LA ISRAELI
1.Wanawake walioingia kwenye taifa la
Israeli,wanawake aliowependa Mfalme Sulemani walimgeuza moyo alipokuwa mzee na
hakumfuata Bwana Bali miungu.
(1 Wafalme 11:4)
Jambo la kujifunza:Wanawake wale walimgeuza
moyo alipokuwa mzee,maana yake ni kwamba shetani aliwategesha pale kwenye taifa
kwa muda na baadae wakawa mtego kwa Mfalme, ni muhimu ukafahamu kuwa ni muhimu
sana kuiombea idara ya uhamiaji hususani katika suala la utoaji vibali vya
kuishi nchini ili Mungu awawezeshe katika masuala ya utoaji wa vibali ili
wasije wakampa kibali mtu ambaye ameletwa na shetani katika taifa ili awe mtego
kwa taifa.
2.Wanawake wageni walimfanya Sulemani
akajenga madhabahu za miungu katika taifa jambo ambalo ni machukizo kwa Bwana.
(1 Wafalme 11:7)
Kumbuka Mfalme anapojenga madhabahu za miungu
hajengi kwa pesa same za mfukoni Bali anatumia rasilimali za taifa kwa hiyo kwa
kufanya hivyo anaukabidhi uchumi wa taifa kwa miungu na si ajabu kukuta bajeti
kubwa inaelekezwa kwenye ujenzi wa viwanda vya pombe,sigara,upanuzi wa magereza
n.k na taifa zima linaingia kwenye hatia ya kuabudu miungu.
3.Ufalme wa Sulemani,Mungu aliugawanya lakini
ni katika siku za mwanae(1 Wafalme 11:11-12)maana yake ni kwamba taifa
liligawanyika lakini kosa lilifanywa na Mfalme Sulemani.
(1 Wafalme 11:9-11)
Jambo la kufahamu jaribu kuchunguza mataifa
mbalimbali yaliyogawanyika;Sudani,Korea n.k ni rahisi sana kukuta chanzo cha
mgawanyiko ilikuwa ni safari mbalimbali kwa mfano unaweza kukuta kiongozi
alisafiri na katika ziara yake akanyweshwa maneno na aliporudi akaongoza
mapambano ya kupindua serikali,fuatila kuhusu mataifa mbalimbali kwa mfano
Uganda utaona Raisi Milton Obote aliwahi kuishi hapa Tanzania na akatengenezwa
na aliporudi Uganda akachukua nchi kijeshi.
4.Mfalme Sulemani akataka kumuua Yeroboamu
mtu ambaye Bwana alimuandaa kuwa Mfalme,maana yake ni kwamba baada ya Sulemani
kugeuzwa moyo wake ghafla akawa na uchu wa madaraka hivyo basi hakuwa tayari
kuona mtu baki akiwa Mfalme ingekuwa kwa nyakati za sasa tungeweza kusema kuwa
Raisi hayuko tayari kuachia madaraka kwa mtu asiye wa chama chake anachohitaji
ni kwamba hata akitoka madarakani atawale mtu wa kutoka kwenye chama chake.
Ni muhimu sana kuombea safari za watu
mbalimbali iwe viongozi au wasio viongozi kumbuka yote hayo uliyoyasoma
yalitokana na safari za viongozi na wasio viongozi.
MAMBO KADHAA YA KUOMBEA JUU YA SAFARI ZA VIONGOZI
NA WASIO VIONGOZI MAADAMU WANAINGIA NA KUTOKA KATIKA NCHI HUSIKA
1.Ombea mipaka isipitishe kitu chochote
kisicho cha mapenzi ya Mungu
(Mathayo 16:19)
2.Kwa njia ya MAOMBI,funga safari zote za
ndani na nje ambazo zimeratibiwa na shetani (Mathayo 16:19)
3.Ikiwa shetani kuna watu amewategesha nchini
kwako kwa makusudi fulani,omba Mungu awarudishe walikotoka(1 Wafalme 11:1-4)
umeshawahi kufikiri juu ya wapelelezi ambao Musa aliambiwa na Mungu waende
waipeleleze nchi ya Kanaani(Hesabu 13) ni Mungu aliwatuma kupitia MUSA basi ni
vema uelewe kama Mungu alimwagiza Musa kuwatuma watu kupeleleza, ni ujue na
shetani naye huwa anachomeka watu katika taifa wanaingia kama wageni na sio
kwamba ni wageni kweli Bali wanaingia kutekeleza kusudi la shetani, jaribu kuwauliza
waKenya juu ya shambulio la soko la kimataifa la West gate Mall,ukifuatilia
tukio hilo utaona magaidi waliingia wakitokea Somalia na wakafanya uharibifu
mkubwa sana.
4.Omba Mungu avunje umoja uliotengenezwa na
shetani, kumbuka shetani alimuunganisha Mfalme Yehoshafati na wakaunganisha
nguvu za kijeshi ili waende vitani(1 Mambo ya nyakati 18:1-34) matokeo yake
kuna madhara makubwa yalitokea, umewahi kujiuliza juu ya miunganiko mbalimbali
kama SADC,COMESA,UN,EAC(japo miunganiko ya namna hii haiwezi kuvunjika kwa kuwa
inatokea kwa kuwa tunaelekea mwisho wa dunia) umeshawahi kujiuliza ni nani
muhasisi wake? Unayajua malengo yake? Umeshawahi kujiuliza faida na hasara
zake? Umeshawahi kutathmini matokeo ya miunganiko hiyo kwa ngazi ya taifa na
maisha ya mtu mmojammoja kiroho na kimwili?
0 Maoni